Sunday, 23 December 2012

CHAMUITA WAZINDUA WEBSITE YAO



Rais wa (CHAMUITA) Addo November, katikati  Mweka Hazina Upendo Kilahiro  na Naibu Mwenezi John  Shabani.

Na Khadija Kalili

MAPEMA wiki hii Rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania (CHAMUITA)  Ado November ameitaka serikali kutokukimbilia mchakato wa kufanya usajili kwa kazi za wasanii kwa kutumia stika moja bila ya kuweka mipango madhubuti ya kuwabana wezi wa kazi hizo.

Akizungumza jana Dar es salaam November anasema kwamba Serikali isikimbilie katika stika pekee bali watupie kwanza macho ya kazi za wasanii zinazoibiwa sehemu mbalimbali kama kwenye mabasi, ambako huoneshwa filamu na CD za miziki ya Injili huku msanii akiachwa bila ya kupata faida yeyote.

“Sio hao ntu bali wezi wengine ni pamoja na waumini wakuu wa  dini ya Kikristo kwani nao utawaona wakitoka katika nyumba za kuabudu Kanisani wanalipia fedha kidogo huku wakidurufiwa CD huku wakichagua ,majina ya wasanii  wanaotaka nyimbo na picha zao ,utasikia wakitoa orodha ya majina ya nyimbo na albamu wanazozitaka, katika hili hata mungu hatoweza kupokea sadaka zao wanazozitoa makanisani kwani wanafanya dhuluma kwa watu wanaojinyima na kurekodi lakini wao badala ya kununua albamu nzima wanaishia kuchoma CD” anasema  November.

Anaongeza kwa kusema ,”Sisi  kama CHAMUITA tumejipanga  kuwekeza  katika elimu zaidi ili wasanii wa muziki wa Injili waweze kufahamu haki zao  kwanza kabla ya kuingia katika mpango huo ambao ni mzuri kimaendeleo.

Wakati huohuo November anasema   CHAMUITA wamepiga hatua  kubwa kwani hadi sasa tayari wameshszindua ‘website’  ya chama itakayofahamika kama www.gospal Tanzania.com ambapo wasanii ambao ni wanachama wataweza kujitangaza  kwa kuuza picha, nyimbo na zao kwa kupitia mtandao huo


Wakati huohuo mjumbe wa CHAMUITA , Bahati Bukuku amezungumza kwa niaba ya waimbaji wengine wa muziki wa Injili kwamba serikali sikurupuke katika suala la uanzishwaji wa kutumia stika moja kwani itawabebesha mzigo wasanii na kazi zitaendelea kuibiwa zaidi.


“Wizi wa kazi za sanaa ni janga la Taifa hivyo kila Mtanzania anapaswa alipigie kelele, hiki ni kilio cha umma sisi wasanii hatukubaliani kwamba kila msanii atatumia stika moja , hapo wizi utaendelea kwanini wasitumie mfano wa kadi za benki huku kila mmoja akawa na namba au neno lake la siri ili  kila msanii ajue anakwatwa kodi kwa namna gani  na kwa kutokana na kopi ngapi  kulingana na kipato chake lakini ikiwa stika moja wapo wasanii watakaopandia kwa kupitia jina la mwingine”anasema Bukuku.

MALENGO NA MADHUMUNI
November anasema CHAMUITA Itaendeshwa kama chombo kisicho na malengo ya kupata faida na kitakuwa na malengo na madhumuni yafuatayo anayoyataja, Kulinda utamaduni wa Tanzania na heshima ya muziki wa Injili, Kuhamasisha maendeleo ya muziki wa Ijili na nyaja zake nyingine,Kutoa ushauri katika mambo yote yahusuyo muziki wa Injili.Kuwakilisha na kulinda maslahi ya wanachama kitaifa na kimataifa, Kuwa chombo cha kuwezesha mawasiliano kati ya watu na vikundi katika kupeana taarifa kuhusu muziki wa Injili, Kuwa na rejista ya wanamuziki wa Injili na kazi zao.  Ili kusaidia kulinda na kutangaza haki za wanachama, Kutafuta mapato kwa njia ya ada, michango, harambee, maonyesho, kukopa, ufadhili au zawadi katika kuendeleza malengo na madhumuni ya Chama, Kuwezesha mawasiliano ya kitaifa na kimataifa, Kuwawezesha wanamuziki wa Injili kwa njia ya kuwaongezea elimu, Kuinua hadhi ya muziki wa Injili nchini,Kutambuliwa rasmi na Serikali yetu na wadau wengine Tayari tumesajiliwa na BASATA na kupewa usajili rasmi na  Kuwekeza katika miradi, na kujipatia kipato kwa nia ya kuwakomboa jamii ya wanamuziki wa injili.

 Changamoto kwa wasanii

Wasanii mbalimbali ambao walihudhuria mkutano uliratibiwa na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA), walilazimika kutofikia muafaka katika mkutano huo na baadhi ya viongozi waliofika kuzungumzia mpango wa uwekwaji wa stika ifikapo mwakani.

Chama chetu kinaundwa na Mwanamuziki mmoja mmoja yaani solo artist, vikundi, umoja wa Makundi yote ya Muziki  wainjili hapaTanzania, kwa kuhusisha radio, watangazaji, wapigaji na wadau wa muziki wa injili.

Safu ya uongozi (CHAMUITA ) Addo November ,Makamu Mchungaji Joseph Malumbu , Katibu  David Robert ,  Katibu Mwenezi  Stella Joel, Naibu Mwenezi John  Shabani, Mweka Hazina Upendo Kilahiro.

Wajumbe wa Kamti Kuu  wako zaidi  ya 60 huku baadhi ni  wakiongozwa na  Mbunge Matha Mlata, Mzee  Makassy, Cosmus Chidumule, Bahatgi Bukuku, Ency Mwalukasa, Christine Shusho, Levina Steven, Mzee Mutash, Jojo Josee , Jackson Bent, Fred Rwesasira.

Mikakati ya Chama
November anasema kuwa tayari wameshazungumza na wanachama wao ikiwa ni pamoja na kuweka mikakati ambayo wamejiwekea ambayo ni kuunganisha wanamuziki wote wa injili na wadau wao na kuwapa nguvu katika majukumu yao ya kila siku, pamoja na kutetea haki za msingi za wanamuziki.

Kuwakumbusha wanamuziki juu ya umuhimu wa CHAMA na kuishi maisha ya kumpendeza Mungu, Kutetea haki za wanamuziki na kutoa wito kwa jamiii na serikali kwa ujumla wa kutambua wizi wa kazi za sanaa kama janga la kitaifa kwani wanamuziki wanakosa mapato na serikali inakosa kodi ambayo inaweza kuzidi hata mapato ya maliasili na utalii au madini, mfano kazi moja tu ya mwanamuziki mmoja akauza nakala milioni 4 kati ya watanzania milioni 40 waliopo mwanamuziki huyo anaweza kupata bilioni 4 kwa kanda ya shilingi 1000 tu.

November  anasema tunaungana na kauli hii ya Shirikisho la Muziki Tanzania kuwa umefika wakati sasa wanamuziki tuseme basi katika kuibiwa kazi zetu  za sanaa , tunawataka  viongozi  wan chi wakae  pamoja  nasi tuwape mikakati yetu  wasikae mbali  na sisi kwani tuna uwezo  wa kukuza uchumi.
Kutoa mafunzo kwa wanamuziki kuhusiana na muziki na haki miliki, pamoja na kuwekeza katika maisha  ya baadaye  tayari kuna wadau kutoka LAPF  tayari wametoa mada na kuandikisha wanachama, hii ni fursa kwao kujipatia mikopo ya nyumba na kuwekeza katika akiba yao ya baadae.
Kutoa mapendekezo juu ya mabadiliko ya sheria yetu ya haki miliki ambayo kiukweli haina meno na imepitwa na wakati. Leo tunatoa dukuduku chetu juu ya Sheria inayolinda kazi za wanamuziki na wasanii wengine (The Copy Rights and Neighbouring Act no 7 of 1999) mfano suala la faini isiyozidi milioni tano, kwani sheria haisemi kazi hizo feki zinapelekwa wapi na faini hii imekuwa ndogo mno na pia inatoa mwanya kwa watafsiri sheria ambao mara nyingi tumejionea wakitoa hukumu ya mwizi kulipa faini ya laki mbili au elfu sabini na kurudishiwa kazi yake ya wizi maana sheria ipo kimya.
Tunatoa pongezi wa Rais Kikwete kwa kukubali mchango wa Chama mcha muziki wa injili na kukubali kuwa chama pekee kilichoshiriki kuimba katika miaka 50 ya uhuru pale uwanja wa taifa.
Hata hivyo tunatoa rai kwa viongozi wa serikali kushirikisha makundi mbali mbali ya sanaa katika mchakato mzima wa kutetea haki za wanasanaa wote kwani hiii itawapa fursa kufanya mambo yatakayokidhi haja za wanamuziki na sanaa kwa ujumla.
Tunawashukuru wanamuziki wa injili na wdau mbali mbali kwa jinsi walivyojitoa katika kumzika mzee wetu, Remmy Ongala, waandishi waliopata ajali wa radio za injili ambapo chama kilijitoa kuwaona na kuwafariji,  msiba wa Fanuel Sedekia na kusaidia waathirika wa Gongo la Mboto kazi hii ilifanyika kwa ufanisi mkubwa na mzee wetu Remmy alizikwa kwa heshima kubwa, tunawaomba tuzidi kushikamana.
“Tunashukuru  sasa tumezindua uzinduzi website ya kwanza kutoka kwa wanamuziki wa Tanzania, ambayo ni www.tanzaniagospel.com iliyotengenezwa na Kampuni ya Spice Olyympus.
 pamoja na haya bado tunajipanga kuwatafutia wanamuziki wa injili mafunzo zaidi ya kuwafanya kujitegemea na kusaidia maendeleo ya nchi” anasema November

Mwisho November anamalizia kwa kutoa pongezi za dhati na shukrtani kwa LAPF kwa kudhamini mkutano wao  na kuwaomba wanachama kuwaunga mkono katika jitihada  zao za kuwa komboa  watanzania.

No comments:

Post a Comment