Wednesday, 12 December 2012

RAY C AMSHUKURU RAIS KIKWETE KWA MATIBABU


 
MSANII wa muziki wa kizazi kipya  (Bongo fleva) Rehema Chalamila ‘Ray C’, juzi ametinga Ikulu kufikisha shukurani zake kwa Rais Jakaya Kikwete kutokana na kumpatia msaada wa matibabu.
Ray C aliyefuatana na Mama yake Mzazi Margareth Mtweve na Dada yake Sarah Mtweve, alimweleza Rais kuwa afya yake imeimarika na kwamba muda si mrefu atarejea jukwaani kwa ajili kukonga nyoyo za mashabiki wake waliyomkosa kwa muda sasa.
Kwa apande wake, mama mzazi wa Ray C, alisema anamemshukuru Rais Kikwete kwa kuokoa maisha ya mwanaye kwani hali ili kuwa ya kusikitisha wakati alipokuwa akiumwa.
Aidha mama Ray C amesikitishwa na baadhi ya watu kutumia fursa ya matatizo ya mwanaye kuwa chanzo cha kujipatia fedha kwa kukusanya michango eti  kwa ajili ya matibabu.
Mama Ray C aliongeza kwa kuwataka baadhi ya watu amnbao wanafanya vitendo hivyo kuacha mara moja kwa kuwa kwani matibabu ya Ray  C yamegharamiwa na Rais.

No comments:

Post a Comment