Sunday, 23 December 2012

MUIMBAJI WA MUZIKI WA IN JILI ALIYEDHALILISHWA KIJINSIA


DONNIE Mc Clurkin ni Mwanamuziki Mashuhuri wa nyimbo za Injili na Mchungaji wa Kanisa la Perfecting Faith church lililopo katika jimbo la Detroit nchini Marekani.
Donnie alizaliwa na familia ya Donald na Mama Frances Mcclurkin Januari 25, mwaka  1959 na kukulia katika mji wa Louisville.
Akiwa na umri wa miaka nane, mdogo wake wa kiume mwenye umri wa miaka miwili aligongwa na gari na kufa papo hapo huku Donnie akishuhudia.
Wakati Donne akiwa na majonzi mazito usiku huo huo ambao walimzika mdogo wake, mjomba wake alimbaka Donne.
Baada ya kifo hicho familia yake iliingia kwenye mgogoro kubwa ambao ulitokana na utumiaji wa dawa za kulevya.
Muimbaji huyo alipofikisha miaka 13, binamu yake mtoto wa mjomba wake alimbaka tena Donnie pamoja na dada zake wawili kitendo amabacho kilimuumiza sana na kumuachia kovu la aina yake.
Anasema kuwa muda wote alijiona mkosaji, mtu aliyekandamizwa na hakuwa na ujasiri mbele za watu na mwenye wingi wa aibu.
Kwa kipindi hicho chote anaeleza kuwa alipata faraja toka kwa shangazi yake ambaye alikuwa muimbaji wa nyimbo za Injili.
Shangazi yake huyo alimfanya Donnie ajiingize kanisani na kuanza kupiga piano na kuimba kwaya kama sehemu ya kufuta machungu na kuondokana na msongo wa mawazo aliokuwa nao.
Mama yake mzazi naye alikuwa muimbaji kanisani hivyo kanisani kukawa ndio nyumbani kwake na kambi yake pindi nyumbani kukitokea matatizo.

Julai 14, 1969 akiwa na miaka takribani kumi ikiwa ni jumapili akiwa kanisani huko Amityville Gospel Tabernacle mtumishi wa Mungu aliyekuwa akihubiri aliwaambia watu kuwa Kristo alikufa kwa sababu anakupenda wazo  hilo ndilo lilikuwa kwa Mcclurkin ndipo akaamua kuyakabidhi maisha yake kwa Yesu.
Kwenye kitabu alichoandika kuhusu maisha yake anasema “ Kanisa limekuwa ndio ulimwengu wangu mahali ambapo najisikia amani na najisikia kama ndio Mahali Pangu halisi”anaeleza.
Mwaka 1971 wakati ana miaka 11, alikuwa akimpenda sana mwanamuziki mashuhuri wa nyimbo za injili kipindi hicho aliyeitwa Anre Crouch.
Anaeleza kuwa siku aliposikia kuwa Crouch anakuja katika jimbo lao alimuomba mama yake ruhusa waende kwenye tamasha na kumuahidi jumatatu yake ataamka mapema na kwenda shule kama kawaida.
Anaendelea kusema kuwa mama yake alikubali na wakaenda Tamashani na Donnie akaaa mbele kabisa sambamba na mamaye.

Baada ya Crouch kuingia ukumbini saa tano usiku kabla hajaanza kuimba alimuona Donnie na kumfata, Donnie anasema, “Crouch akaniuliza kitu gani unafanya hapa, nikamjibu nakusubiri wewe, akaniuliza kama nimelipenda tamasha nikamjibu ndio, akanambia wakati yuko mdogo hakuweza kuimba wala kucheza mpaka baba yake alipomuombea, Nikamjibu baba yangu hajaokoka hivyo hawezi kuniombea. Mwishoni akaniuliza kama nitapenda aniombee nami nkamkubalia akaweka mkono wake kichwani kwangu akasema “Mungu mpe kile ambacho umenipa mimi” kisha akaelekea stejini, huuo ulikuwa ndio mwanzo wa hiki nlichonacho leo”anasema Donnie.

Akiwa kanisani hapo alianzisha kundi llilokuwa linajulikana kama The Mcclurkin Singers na baadaye alianzisha kundi lililokuwa likijulikana kama The New York Restoration Choir.
Mwaka 1983 wakati akiendelea kutumika na kwaya alikutana na Pastor Marvin Winans.
Mchungaji Winans alivutiwa sana na namna Donnie alivyokuwa akiimba kwenye semina ya injili.
Baadaye Winans alimwalika Mcclurkin katika mji wa Detroit alikokua akiishi ili kumsaidia kuanzisha huduma kanisa liitwalo Perfecting Faith Church.
Miaka sita baadaye Donnie aliamua kuhamia Detroit na kuanza kufanya kazi na Pastor Winans.
Katika kipindi hicho anasema kuwa ndipo Mcclurkin alipata wasaa wa kuzunguka sehemu mbalimbali na kufanya huduma akiwa chini ya pastor Winans.
Donnie anasema familia ya Winans imekuwa karibu sana na yeye Kuanzia Bebe, Cece, na Pastor Marvin na wakati mwingine anafikiri yeye ni Donnie Mcclurkin Winans.
Donnie Mcclurkin na Cece Winans wakiwa wameshikilia tuzo za Trumpert awards walizopewa mwaka 2007
Akiwa na Pastor Winans, alisaini mkataba na kurekodi albamu yake iliyoitwa LP, Albamu hiyo iliyokuwa na nyimbo kama Stand iliyongoza kwa umaarufu na kuzinduliwa na Oprah Winfrey.
Nyimbo hiyo ilitunukiwa tuzo ya Grammy kwa mwaka huo wa 1996 kwa upande wa nyimbo za Injili. Album zake tatu za solo zilikamata nafasi za juu sana kwenye chati za Bilboard.
Akiwa na furaha ya ajabu Mcclurkin kupitia makongamano mbalimbali huwasimulia watu ukweli wa maisha yake huku akipinga kwa nguvu mahusiano ya jinsia moja.
Mcclurkin anaamini kwamba suala la Homosexuality ni suala la kiroho haliwezi tibika kisaikolojia na linahitaji msaada wa Mungu pekee. Baada ya watu wengi kuwa wanamuomba aelezee historia ya maisha yake, Mcclurkin aliamua kurudi nyumbani kwao Amityville New York na kumuomba Mama yake ruhusa ili aandike kitabu kuhusu maisha yake.
Frances Mcclurkin (mamaye), alimruhusu Donnie aandike kitabu kinachoyaelezea maisha yake kinaga ubaga, ndipo Mcclurkin akatumia miezi 18 kuandika kitabu hicho ambacho alikiita Eternal Vitcting, External Victor. Alisema aliamua kuandika kitabu sio kwa kusudi la kuweka wazi uovu uliokuwa ukifanyika ndani ya Familia yao bali kwa sababu yeye ni Mwalimu, na mwalimu ni vizuri ajitoe yeye kama ujumbe ili watu wengine wajue kuwa hawako peke yao kwenye mambo wanayopitia.

Mwaka 2008 Mcclurkin alichaguliwa kuwa miongoni mwa wanamuziki ambao watakuwa kwenye timu ya Barak Obama katika harakati za uchaguzi wa nchini Marekani.
Mcclurkin alikubali na kujumuika na Barak Obama, lakini kutokana na msimamo wake wa kupinga mahusiano ya jinsia moja, Mashoga wengi walipinga kuwepo kwake kwenye timu ya Obama. Hivyo ili kupata kura za mashoga ilibidi Mcclurkin atolewe kwenye orodha hiyo ingawa alifanikiwa kuimba kwenye moja ya kampeni za Rais Obama
Makala hii imeandikwa kwa msaada wa mtandao na Happiness Mnale, 0712 00 35 39,barua pepe mnaleh@yahoo.com
mwisho

No comments:

Post a Comment