MSANII Antoine
Agbepa Mumba almaarufu kama Koffi
Olomide (56) ambaye ni
mahiri katika uimbaji wa miondoko ya
Soukous yupo nchini kutoa burudani Jumamosi Desemba 15 2012.
Ni msanii mwenye
majina mengi yaliyompa umaarufu kama Grand Mopao, Mokonzi, Tcha Tcho king,
atatumbuiza na bendi yake ya
Quartin Latin katika uwanja wa Leaders
Club Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Akiwa nchini
kwa uratibu wa Kampuni ya Prime Time
Promotions Olomide ametua na muimbaji nyota wa bendi hiyo Sindy ambapo
watapamba miaka 13 ya kuanzishwa kwa Kampuni ya Clouds FM.
Mbali ya bendi ya Koffi pia bendi pinzani nchini FM
Academia ‘Wazee wa Ngwasuma’ wakiwa chini ya uongozi wa Kyala Matala ‘Nyoshi El
Saadat’ watatoa burudani sanjari na bendi ya The African Stars Entertainment
‘Twanga Pepeta’ nao wamesema kwamba wamejipanga kwa kutoa burudani kesho.
Akizungumza jana Kiongozi wa Twanga Luiza Mbutu anasema
kwamba watatumia onesho hilo kwa kujifunza muziki kutoka kwa Koffi kwani kundi
hilo linaongozwa nha nguli wa muziki
duniani.
Aidha katika hali nyingine haijawahi kutokea kwa bendi
mbili pinzani za Twanga na FM Academia kupanda katika jukwaa moja na onesho
moja hivyo siku ya kesho itakuwa ni siku maalumu kwa
wapenda muziki kupata burudani kutoka kwa bendi mbili kubwa nchini na moja ya
kimataifa.
Bendi nyingine itakayosindikiza katika onesho hilo ni
Skylight iliyozinduliwa mwaka
huu.Kiingilio ni sh.10,000 kabla na sh. 15,000 mlangoni.
Alikotoka
Koffi Ambaye ni mwanamuziki mahiri msomi pia mtunzi
mzuri wa nyimbo amabye alianza kuonesha
umahiri wake kati ya mika 1970 na 1980 ambako alikua akimuandikia nguli wa
muziki nchini Janhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Papa Wemba enzi hizo akiwa na
bendi ya Orch Viva La Musica.
Wakongomani wengi
wanamkubali Koffi Olomide kuwa yeye ni
chuo cha mafunzo kwa wanamuziki wengi wa DRC, mmoja wa wanao ukubali ujabali wa
muziki wa Olomide ni pamoja na mwanamuziki wa kikongo anayeishi jijini Nairobi
nchini Kenya Kasongo wa Kanema anayetumikia katika bendi ya Super Mazembe
hukuakisema “Koffi ni msafi katika muziki na tungo zake pia kwani ujumbe
anaoutoa unakuwa wenye uzito na maana kubwa”.
“Nyimbo nyingi za
Olomide ziko kipekee na ikipigwa tu utatambua kuwa sasa mopao yuko hewani,kutokana
na ujuzi wa aina yake mpangilio
murua ndio unaompatia mrehjesho mzuri,
kuuza vema kazi zake na kumpatia umarufu”anasema Kanema.
Kasongo anasema
kwamba kupendwa kwa muziki wa Koffie sio kwamba kumekuja bure amesoma ,
amejituma na huumiza kichwa kila anapotaka kuachia albamu hio ndiyo siri kubwa
ya muziki wa Koffie.
Kwa wadau wa
muziki watakumbuka moja ya kibao kilichotamba kuwa ni 'Papa Plus', 'Futa
Djalon', 'Andraa', 'Loi', 'Mbirime', 'Micko', 'Attentat' na 'Ngounda'.
Pia Koffi amewahi kurekodi na mwanamuziki Nyboma
Mwanindo wimbo wa 'Anicet' na 'Papa Bonheur'
Changamoto katika muziki
Kwa muda wa miaka mitatu
iliyopita mwanamuziki huyu hakuweza
kufanya maonesho barani Ulaya kutokana nakukabiliwa na kesi ya kunyanyasa
wacheza shoo wake huku wakihusishwa na masula ya kisiasa anti-Kabila.
Koffi aliwekwa
chini ya ulinzi Agosti 15, jijini Kinshasa, pia alitetewa na jopo la mawakili
wapatao 10.
Kama ilivyo
kawaida ya wanamuziki siku zote kusaka maslahi yao ,mwaka 1998 Koffi alionja
chungu ya muziki baada ya onesho kubwa
lililofanyika kwenye ukumbi wa Olympia jijini Paris bendi yake ilivunjika.
Ilivunjwa na
baadhi ya wanachama na wanamuziki walioenda kuanzisha bendi ya Orchestre Quartier Latin Academia.
Historia yake kwa ufupi
Alizaliwa Julai13,
1956, Kisangani kabla familia yake haijahamia Kinshasa DRC huku mama yake akiwa
mwenye asili ya huko na baba yake ni mwenye asili ya kutoka nchini Sierra Leone.
Ametoka katika
familia yenye maisha na uwezo wa kati
Mwaka 1970 akitokea nchini Ufaransa alijiunga na bendi ya Viva la Musica iliyokuwa ikimilikiwa na Papa Wemba ambapo alikuwa katika nafasi za ‘
music composer’ na mwandishi wa nyimbo na baadaye akaja kuwa mwimbaji mahiri.
Mwaka 1986, alilipa
kisogo kundi la Viva la Musica na
kuanzisha bendi yake ya Quartier Latin,ambayo
ilikuwa imesheni ala zote za muziki,
waimbaji, na wacheza shoo huku kundi
zima likiwa na wanamuziki wapatao 30.
Kuanzia hapo Koffi
ndipo alipokunjua makucha yake na kujijengea jina Afrika Mashariki, Kati,
Kusini na Afrika Magharibi akitamba na Tcha Tcho mtindo wa soukous.
Mwaka 2002 alipata
tuzo ya muziki ya Kora Award akiwa kama
mwanamuziki bora Barani Afrika.
Mafanikio
Wanamuziki wengi
wenye asili kutoka nchini DRC wengi
wamepita katika mikono yake kama vile Fally
Ipupa, ambaye Koffi alimpika kwa muda wa miaka 10 ndani ya bendi yake ya Quartier Latin , kabla
mwanamuziki huyo hajaamua kua solo na hatimaye kuanzisha bendi yake.
Kwa sasa Fally ni kati ya
mwanamuziki wenye heshima na jina kubwa duniani ambaye anafanya kazi na
kuisshi nchini Marekani huku akifanya kazi kwa karibu na G-Unit of 50 Cent’s
Olivia.
Nyota mwingine
katika muziki aliyepitia katikia mikono ya Koffi ni Ferre Gola, baada ya
kuachana na kundi la Werra Son Wenge Musica Maison Mere.
Kama hiyo
haitoshi tunda lingine adhimu la kazi ya
Koffi ni Montana Kamenga ambaye baada ya kujiona amewiva kimuzi kutoka kwa
Koffi alikimbilia kwa General Defao Matumona.
Pia wengine
waliopikwa na Koffi ni Fele Mudogo, Sam
Tshintu, Suzuki 4x4, Buro Mpela na Soleil Wanga.
Kutokana
na umahiri wake katika muziki Koffi amewahi kushirikishwa katika miradi mbalimbali ya muziki ikiwa ni pamoja
na ‘Salsa music project’, ‘Africando music project’.
Albamu:
Effrakata, Tcha Tcho, Magie, Haute De Gamme- Koweit, Rive
Gauche, Pas de Faux Pas, Live A Bercy, Attentant, Ngounda, Le Rambo du Zaire,
Golden Star, Noblesse Oblige, V12, Ultimutum,
Loimore, Monde Arabic na Abracadabra inayotamba hivi sasa.
No comments:
Post a Comment