MSANII Costa
Siboka 'Mfalme wa muziki wa asili' katikati akicheza na watoto alipofanya ziara yake wakati wa sherehe za
Krismas mjini Moshi.
Ambapo alifanya utambulisho wa wimbo wake mpya unaokwenda kwa jina la 'Watoto Wangu' ndani ya ukumbi wa kisasa unaokimbiza Mo-Town unaoitwa Zumba Land .
Costa alifanikiwa kuwapagawisha wakazi wa Moshi kwa kiasi kikubwa ambao kwa
kiasi kikubwa waliongozana na watoto wao hata kumfanya ashangiliwe kila dakika.
Costa Siboka ameahidi kuusambaza uhondo huo katika mikoa ya Iringa, Mbeya na Songea kuanzia mwisho wa mwezi Machi mwakani (2013).
Aidha, Mfalme huyo ameahidi kuimba nyimbo zingine kupitia makabila ya Kihehe, Kinyakyusa, Kingoni na nyingine.
Msanii huyu nyota aliyewahi kutwaa taji la Mr Guiness ukanda wa Afrika Mashariki, amekuwa akipata udhamini wa nguvu toka kampuni kubwa ya bia nchini (TBL), Konyagi na Precision Air.
No comments:
Post a Comment