Na Khadija Kalili
ILIKUWA ni siku ya aina yake
ambapo licha ya kuwa na hali ya hewa ya mvua iliyonyesha na kusababisha muziki
wa bendi ya Skylight iliyokuwa ikitoa burudani nje ya ukumbi wa Club hiyo
lakini mashabiki bado waliendelea kuingia
na kujumuika kwenye sikukuu hiyo.
Mbali na mvua mashabiki hao
ambao walijumuika katika maadhimisho hayo ambayo yamefanyika sambamba na
maadhimisho ya miaka 13 ya kuanzishwa kwa Kampuni ya Clouds FM.
Usiku wa Jumamosi Desemba mosi utabaki kuwa ni siku ya kumbukumbu maalumu ya kutimiza miaka 20 ya Club Bilicanas ambayo pasina shaka ni Club inayotajwa kuwa ni yenye hadhi ya Kimataifa Barani Afrika na hata Ulaya.
Katika sherehe hiyo ambayo
keki ilikatwa na mfanyakazi aliyedumu kwa kipindi chote hicho kwenye Club hiyo
ambaye ni Monica almaarufu kama Da Monica huku wengine wakimwita Mamdogo
alikata na kumlisha Mkurugenzi wa Kampuni ya Bilicanas Group Dk. Lilian Mtei
Mbowe.
Mbali ya tukio la kukata keki
na kumlishana Mkurugenzi pia wadau
mbalimbali waliohudhuria tukio hilo nao pia walipata fursa ya kula kipande
hicho cha keki .
Akizungumza na Tanzania Daima
nje ya ukumbi huo mmoja wa Wakurugenzi
wa Clouds FM Ruge mutahaba anasema
kwamba ni jambo la kumshukuru mungu kwani kwa Kampuni zote hapo zilipofikia
zimepitia changamoto nyingi na siyo jambo rahisi.
Kuanzisha Kampuni na hasa
katika masula ya burudani siyo kazi rahisi hata kidogo jambo kubwa ni namna ya
kuiendeleza ndiyo kazi kubwa.
Kadhalika baadhi ya wadau
mbalimbali wa tasnia ya burudani nchini ambao waliweza kufanya mahojino na Tanzania
Daima wanasema kwamba wanatoa pongezi za dhati kwa uongozi wa Club Bilicanas
kwani tangu kuanzishwa kwake miaka 20 imeweza kufungua milango ya kutoa ajira
kwa vijana wa kitanzania.
Naye Mkurugenzi wa Kampuni ya
The African Stars Entertainment (ASET), Asha Baraka anasema kwamba yeye binafsi
anakumbuka namna Club Bilicanas ilivyoweza kujizolea umaarufu tangu
ilipoasisiwa huku na yeye akiwa ni kati ya wadau na mashabiki wakubwa wa Club
hiyo.
“Nakumbuka namna Club
Bilicanas ilivyokuwa ikitoa raha kwa mashabiki wa hapa Jijini Dar es Salaam na
hata nje ya jiji na kuweza kuvuka mipaka
hadi nje ya nchi” anasema Asha.
Binafsi nina kila sababu ya kuishukuru Club Bilicanas kawani ndani ya miaka 20 tumekuwa tukifanya kazi
kila siku ya Jumatano katika usiku wa Mwafrika ‘Africa Nite’ hivyo kuweza
kugawana riziki kwa namna moja ama nyingine.
Asha anasema katika miaka ya
nyuma Club Bilicanas iliweza kuvumbua
vipaji vya kundi la kunengua la Bilibums ambalo liliwavumbua wanenguaji mahiri ambao ni Hassan Mussa ‘Super
Nyamwela’ ambapo pia alikuwepo aliyekua mnenguaji mahiri Aisha Mbegu ‘Queen
Aisha aliyeitumikia kwa miaka kadhaa
bendi ya Twanga Pepeta .
Kwa sasa wote baada ya kung’ara
na kundi hilo waliweza kuchukuliwa katika
bendi mbalimbali ikiwemo Twanga Pepeta na nyinginezo.
Historia inaonesha kwamba
bendi mbalimbali ikiwemo makundi kadhaa yaliwahi kupamba onesho la usiku wa
mwafrika , usiku ambao umekuwa kivutio kikubwa zaidi ndani ya Club hio .
Baadhi ya bendi zilizowahi
kunogesha usiku huo ni pamoja na bendi ya The Kilimanjaro ‘Wana Njenje’ ambao
wanapiga muziki wao katika mtindo wa mduara.
Shamrashamra za kuadhimisha
miaka 20 ya Bilicanas zitaendelea kwa muda wa mwaka mmoja hadi mwanzoni mwa
mwezi Januari ifikapo mwakani.
Jumapili Desemba 2, ndani ya
Club Bilicanas wazanii nyota wa muziki
wa kizazi kipya walitoa burudani ambao ni Ommy Dimpoz, Linah, Recho,
Amini, Richie Mavoko, Barnaba, Makomandoo, Rais wa Masharobaro Bob Junior na
nyingine mbalimbali.
No comments:
Post a Comment