Sunday, 23 December 2012

NYIMBO ZA INJILI ZILIZOTIKISA 2012


Na Betty Kangonga

UNAPOZUNGUMZIA albamu ya nyimbo za muziki wa injili zilizofanya vema kwa mwaka 2012 ni pamoja na iliyoibwa na mwimbaji wa nyimbo za injili ambaye anakuja juu anayefahamika kuwa ni Enock Jonas.

Moja ya nyimbo inayofanya vizuri na ambayo imekuwa ikipigwa katika sherehe mbalimbali na hata hafla ni ile inayokwenda kwa jina la  wema wa Mungu ‘Zunguka Zunguka’.

Jonas ambaye katika albamu hiyo amefanikiwa kutunga nyimbo zingine nane ambazo ni ufanikiwe, ukimtegemea Mungu, Haleluya
nakuabudu Bwana, ndugu zangu, ni vyema na ile inayosema leo ni furaha.

Mwimbaji mwingine ambaye albam yake inaendelea kufanya vema ni malkia wa nyimbo za injili nchini Rose Mhando ambaye aliitambulisha album yake ya nne inayokwenda kwa jina la Utamu wa Yesu.

Albam hiyo ambayo inafanya vema katika vituo mbalimbali vya redio na televisheni za ndani na nje ya nchi.

Mhando katika nyimbo yake ya Utamu wa Yesu na raha ya ajabu anasema “Nimeonja utamu wa Yesu, Ukitaka gari nzuri, majumba mazuri onja utamu wa Yesu”.

Kama usemi mmoja unavyosema kuwa aliyenacho anaongezewa ndivyo ilivyokuwa kwa mwaka huu kwa upande wa malkia huyo kwani aliweza kuingia mkataba mnono na kampuni ya Sonymeingia mkataba mnono na kampuni mahiri katika masuala ya muziki na burudani hapa ulimwenguni,Sony Music.

Rose Muhando ambaye anakuwa msanii wa kwanza wa muziki wa injili nchini Tanzania kuingia mkataba wa kampuni ya Sony Music, ambayo itamsimamia kutoa album tano hiyo ikiwa ni pamoja katika suala zima la uandaaji na usambazaji.

Kampuni hiyo imedhamiria katika kuwawezesha wasanii wa hapa nchini na imekuwa ikifanya hivyo kwa wasanii mbalimbali duniani ikiwemo wale maarufu kama vile Usher, Chris Brown, Toya Delazy, Beyonce, Pitbull, Tumi and the Volume, J Cole and R Kelly.

Hakika unaweza kuwa mwaka wa bahati na Mungu ameendelea kumwinua mwanamuziki huyo.

Mwimbaji mwingine wa muziki wa injili nchini ambaye  nyimbo zake zimeendelea kukonga nyoyo za Watanzania ni Christina Shusho mbali na kuzindua albam ya nipe macho mwishoni mwa mwaka jana pia alibahatika kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kuwania tuzo za ‘Africa gospel music awards  Julai 7 mwaka huu huko jijini Uingereza.

Pia Shusho kutokana na umahiri wake katika kuimba nyimbo za Injili umemuwezesha kutambulika vyema na kujinyakulia tuzo mbalimbali ikiwemo Tuzo aliyopata huko Nairobi, Kenya.

Shusho alikuwa kati ya wasanii wa nchini waliopata Tuzo za Muziki za Afrika Mashariki na Kati (EMAS) zilizofanyika Agosti 20, mwaka huu na kushirikisha wasanii mbalimbali wa kutoka nchi nane za Afrika Mashariki na Kati.

Mwimbaji huyo aliibuka na Tuzo ya Msanii Bora wa Kike wa Nyimbo za Injili akiingia na wimbo wake unikumbuke na kumshinda mwimbaji mwenzake kutoka nchini Upendo Nkone aliyeingia na wimbo wake Haleluya Usifiwe, Alice Kamande kutoka Kenya na wimbo wake Upendo na Gaby kutoka Rwanda na wimbo wake Amahoro.

Kati ya nyimbo ya Shusho ambayo imeendelea kufanya vizuri ni ile ya kuabudu iitwayo ‘nataka ushirika na wewe’ pamoja na wimbo unaosema ‘Nina wimbo’ ndizo zinazoongoza kuchezwa katika televisheni na redio mbalimbali nchini na nje ya nchi.

Pia mwimbaji wa mwingine wa injili kutoka nchini Kenya Solomon Mukubwa ambaye Aprili 8, 2012 alizindua albam yake inayokwenda kwa jina la ‘Kwa Utukufu wa Mungu’ yenye nyimbo nane na inayoendelea kufanya vizuri ni inayokwenda.

Nyimbo zilizomo katika albam hiyo ni pamoja na Kwa utukufu wa mungu wenyewe ambayo imebeba albam, Usikate tamaa, Mungu wangu Nitetee, Moyo wangu mtukuze bwana, Niko wa Yesu, Mke si nguo, Yesu jina zuri na Chunga ahadi yako.

Mwimbaji mwingine wa muziki wa injili ambaye ameweza kufanya vizuri ni Bahati Bukuku ambaye ameweza kutambulisha albam yake ya  Dunia Haina Huruma iliyobeba nyimbo nane ambazo ni Wewe ni Baba, Dunia Haina Huruma iliyobeba albam, Ahabu,Maamuzi, Atakushangaza, Abneli, Mbeba Maona na Kampeni

Aidha mwambaji Martha Mwaipaja anaweza kuwa ni mwimbaji aliyefanya vyema katika muziki wa injili baada ya kutamba kwa muda mrefu na albam yake ya ‘Usikate Tamaa’ na mwaka huu kuachia album yake mpya inayobebwa na wimbo wa Ombi langu kwa Mungu

Nyimbo zilizomo katika album hiyo ni ile inayobeba albam ya ‘Ombi langu kwa Mungu’ nyingine ni Jaribu kwa mtu, Adui wa mtu, Yesu ni mzuri, kweli nimetambua, kaa na mimi tena, nani ajuaye maumivu, pamoja na sifa zivume huku wimbo wa kaa na mimi tena akiwa amemshirikisha mtangazaji wa Wapo Radio Fm ambaye pia ni mwalimu wa kwaya ya New Jerusalem kutoka EAGT Mito ya baraka Silas Mbise.

Martha ambaye ameolewa machi 4 mwaka huu na mchungaji mchungaji John Said, ambapo inaelezwa kuwa ameweza kupata mafanikio mengi sana kiroho na kimwili kiasi kwamba hawezi kueleza yote.

Wapo waimbaji wengi wa nyimbo za injili walioweza kufanya vema mwaka huu lakini hawa ni baadhi ya wachache ambao kazi zao zinaendelea kuinua mioyo iliyoinama na ile ambayo inaitaji faraja ya Kiungu.

No comments:

Post a Comment